杏MAP导航

Tafuta

2025.04.20Papa akutana na Makamu Rais wa Marekani JD Vance 2025.04.20Papa akutana na Makamu Rais wa Marekani JD Vance  (Vatican Media)

Papa akutana na Makamu rais wa Marekani,Bwana Vance.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ukumbi wa vyombo vya habari Vatican,imetaarifa kuwa Baba Mtakatifu Francisko Dominika 20 Aprili 2025 alikutana katika Nyumba ya Mtakatifu Marta,Makamu Rais wa Marekani,Bwana James David Vance katika mkutano uliodumu kwa dakika kadhaa,ambapo wamebadilishana matashi mema katika siku ya Pasaka.

Vatican News

Dominika asubuhi  tarehe 20 Aprili 2025, muda mfupi baada ya saa5.30, katika nyumba ya Mtakatifu  Marta, Papa Francisko alikutana kwa muda  mfupi wa faragha na Makamu Rais wa Marekani, James David Vance. Hayo yalitangazwa na Ofisi ya Habari, Vatican ikieleza kuwa mkutano huo uliochukua dakika chache, ambao ulitoa fursa ya kubadilishana matashi mema ya  Sikukuu ya Pasaka.

Mazungumzo ya Papa na Makamu Rais wa Marekani
Mazungumzo ya Papa na Makamu Rais wa Marekani   (Vatican Media)

Akiwa safarini nchini Italia na familia yake, Vance vile vile alipokelewa  asubuhi Jumamosi tarehe 19 Aprili 2025, na Kardinali Pietro Parolin, akiwa na Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Mahusiano na Mataifa na Mashirika ya Kimataifa.

Bwana Vance na Kardinali Parolin
Bwana Vance na Kardinali Parolin   (Vatican Media)

Mazungumzo yalikuwa muhimu , ambapo taarifa ilibanisha kuwa yalikuwa na dhamira ya pamoja ya kulinda haki ya uhuru wa kidini na uhuru wa dhamiri ilifanywa upya na kulikuwa na kubadilishana maoni juu ya hali ya kimataifa, hasa juu ya nchi zilizo na vita, mivutano ya kisiasa na hali ngumu ya kibinadamu, kwa umakini maalum kwa wahamiaji, wakimbizi na wafungwa.

Bwana Vance katika ibada ya mateso Ijumaa kuu katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro
Bwana Vance katika ibada ya mateso Ijumaa kuu katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro

Siku ya Ijumaa alasiri, Makamu Rais wa Marekani pia alishiriki, akiwa na mke wake na watoto watatu, Maadhimisho ya Mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican, yaliyoongozwa na Kardinali Claudio Gugerotti, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Makanisa ya Mashariki

20 Aprili 2025, 16:36