杏MAP导航

Tafuta

2025.04.06 Papa akiwa mbele ya madhabahu katika Uwanja wa Mtakatifu Petro Mjini Vatican wakati wa hitimisho la Jubilei ya Wagonjwa na ya Ulimwengu wa Kiafya. 2025.04.06 Papa akiwa mbele ya madhabahu katika Uwanja wa Mtakatifu Petro Mjini Vatican wakati wa hitimisho la Jubilei ya Wagonjwa na ya Ulimwengu wa Kiafya.  (Vatican Media) Tahariri

Ishara ya uwepo katika kipindi cha hali halisi ya mitandaoni

Mwariri mkuu wetu wa Baraza la Kipapa ameandika tahariri yake kuhusu kufika kwa Baba Mtakatifu wakati wa hitimisho ya Jubilei ya Wagonjwa bila kutarajiwa kuwa:“ Ni ishara za uwepo katika wakati wa hali halisi ya mitandaoni:Ushiriki wa Papa Francisko katika Jubilei ya Wagonjwa.”

Andrea Tornielli

Ushiriki usio tarajiwa wa Papa Francisko wakati wa hitimisho la maadhimisho ya kiliturujia ya Jubilei iliyojikita kwa ajili ya wagonjwa na ya Ulimwengu wa kiafya, unawakilisha ujumbe wa kina sana. Hata wakati ambao hali halisi ya mitandaoni,  katika kipindi ambacho tunaamini kuweza kushiriki yote tukibaki nyuma ya skrini ya Komputa, lakini uwepo kimwili ni muhimu sana. Kuwepo kama mtu, kupata ugumu wa kusafiri, wa kutoka, wa kusubiri; wa kufanya uzoefu mgumu wa kutembea, wa kukaribia wengine, wa kutokwa jasho, kupigwa jua au katika anga la wazi,  ni mantiki ya  kukutana na mtazamo wa wale walio karibu nasi, uzoefu wa kuwa na wengine, na kuwa  sehemu ya watu wa mahujaji.

Papa akipta mlango Mtakatifu
Papa akipta mlango Mtakatifu   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Katika ishara ambayo haikutangazwa, Mfuasi wa Petro, anatufundisha kuwa hakutakuwepo kweli na kamwe kinachoweza kubadilisha uwepo wa kimwili, yaani  kuwepo kamili. Kutoka nje  kwa Papa katika Jukwa la Uwanja wa Mtakatifu Petro kwa hivyo,  jambo lenyewe ni ujumbe muhimu zaidi kuliko neno lolote: licha ya sauti ambayo bado dhaifu, licha ya mirija ya oksijeni aliyo nayo, lakini alitaka kuwa hapo.

Kuna maana nyingine ya pili: Papa Francisko alichagua kwa mara ya kwanza baada ya  mwisho wa kulazwa  Hospitalini Gemelli, katika maadhimisho ya Jubilei ambayo anahisi kwa namna ya pekee kuwa karibu: ile ambayo imejikita kwa wagonjwa, ambao wanateseka na kwa wale wanaowahudumia wanaoteseka. Hata kama hatari imepita, Papa Francisko bado anaendelea na kupumzika na matibabu ambapo lakini bado anaonesha ishara za ugonjwa. Ni mdhaifu kati ya wadhaifu ambaye hakukosa kushiriki “Jubilei yake, kwa kuungama katika Basilika na kupita katika Mlango Mtakatifu kama wanavyofanya maelfu na maelfu ya watu kila siku. Mlango ule ambao Papa alikuwa ameufungua usiku wa Noeli, na ambao Jana (6 Aprili) amepita kirahisi kama mhujaji ambaye bado anaendelea kubeba matokeo ya nimonia.

Papa Francisko alishutusha waamini
Papa Francisko alishutusha waamini   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Hatimaye kutoka nje kwa kushtukiza Dominika asubuhi, kunatueleza juu ya uhusiano wa Mchungaji na zizi lake, Askofu na watu wake. Licha ya kuendelea kupona, licha ya maonyo ya madaktari, Papa Francisko hakukosa kukutana na watu, hata kama anatambua hatari inayoweza kutokea kwa ajili ya afya yake. Kwa kufanya hivyo kunatueleza kuwa hata ikiwa wakati mwingine licha ya hali ambayo inaweza kutokea, ya ì muktadha wa kutazama kupitia vyombo vya habari na mtandaoni kwa sababu ya kulazwa, au wakati wa karantini katika kipindi cha janga la Corona, au kutowezekana kusafiri, mkutano wa uwepo halisi,  hauwezi kubadilishwa. Kwa sababu kama alivyokuwa amesema karibu mwaka mmoja uliopita kwamba: “Upendo unahitaji utekelezaji, upendo unahitaji kutolewa, wa kukutana na  unahitaji muda na nafasi ya kutoa: hauwezi kupunguzwa katika maneno mazuri au picha katika skrini…” Na hii inatosha hata ya  upendo wa Papa kwa ajili ya watu wa Mungu ambao daima “amezungumza hata kwa ishara na upole.

TORNIELLI NA PAPA KUFIKU UWANJANI
07 Aprili 2025, 12:22