Timu ya wanariadha Vatican:wanamichezo wanasali kwa ajili ya Papa
Vatican News
"Ave Maria pamoja na Papa na kwa ajili ya Papa" ndiyo kauli mbiu ya Dominika tarehe 2 Machi 2025 saa 2.15 asubuhi, masaa ya Ulaya na saa 4.15 masaa ya Afrika Mashariki na Kati, kabla ya kuanza kwa nusu marathon ya Roma hadi -Ostia, ambapo Timu ya MWanariadha ya Vatican itatoa sauti kwa hisia za ulimwengu wa michezo kuomba kwa urahisi, barabarani kwa ajili ya afya ya Papa Francisko aliyelazwa Hospitalini Gemelli tangu tarehe 14 Februari 2025. Sehemu ya mkutano itakuwa karibu na Uwanja wa Pier Luigi Nervi, mbele ya Jumba la Michezo huko Eur, karibu na sanamu ya miaka ya miatisa ya Arnaldo Pomodoro.
Wazo pia la amani
Kwa mtindo wa Kikundi cha michezo cha Vaticana ambacho ni Chama rasmi cha michezo cha Mji wa Vatican litasali iliyotungwa iitwayo "Sala ya Mkimbiaji wa Marathon" na Salamu Maria kwa ajili ya kumuombea Baba Mtakatifu Francisko kulingana na nia yake, kwa mawazo maalum ya amani mahali popote palipo na vita, hata vilivyosahuliwa. Zaidi ya hayo, Jumamosi tarehe 15 Machi 2025 kutakuwa na mkesha wa Mbio za Marathoni za Roma, Misa ya wanariadha wa mbio za marathoni katika Mwaka Mtakatifu itaadhimishwa, saa 12 jioni masaa ya Ulaya na saa 2.00 usiku masaa ya Afrika Mashariki na Kati katika Basilika ya Arca Coeli huko Campidoglio.