杏MAP导航

Tafuta

Papa anaendelea na matibabu huko Gemelli. Papa anaendelea na matibabu huko Gemelli.  (ANSA)

Papa huko Gemelli,hali tulivu,upokeaji wa hewa ya mitambo umesimamishwa

Papa Francisko anaendelea kupokea oksijeni,hana homa.Utabiri unabaki kuhifadhiwa.Leo asubuhi alihudhuria Misa.

Vatican news

"Hali za kimatibabu za Baba Mtakatifu zimesalia kuwa shwari leo hii; Papa hakuhitaji uingizaji hewa ya mitambo isiyo na uvamizi, lakini matibabu ya oksijeni ya mtiririko wa juu tu; Hana homa.

Kwa kuzingatia ugumu wa vipimo vya kliniki, utabiri unabaki kulindwa.

Asubuhi ya leo Baba Mtakatifu alishiriki Ibada ya Misa Takatifu, pamoja na wale wanaomhudumia katika siku hizi za kulazwa, kisha akabadilishana mapumziko na sala."

Haya ndiyo yaliyoripotiwa katika taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya habari  Vatican, jioni ya leo Dominika  tarehe 2 Machi 2025, kuhusu afya ya Papa, Francisko ambaye amelazwa hospitalini Gemelli Roma tangu 14 Februari.

Hapakuwapo na matokeo ya moja kwa moja ya shambulio la (bronchospasm) kwikwi lililojitokeza la  kipekee siku ya Ijumaa iliyopita. Walakini, inabaki hatari ya kukosoa na kwa sababu hiyo utabiri unabakia kuhifadhiwa.

Imesasishwa mwisho saa 1.30 usiku tarehe 2 Machi 2025.

02 Machi 2025, 19:30