杏MAP导航

Tafuta

2025.03.28 Jengo la anapokaa Papa Francisko"Domus Sanctae Marthae" au Casa Santa Marta". 2025.03.28 Jengo la anapokaa Papa Francisko"Domus Sanctae Marthae" au Casa Santa Marta". 

Papa anaendelea kupata nafuu kidogo,upunguzaji wa oksijeni unaendelea

Papa alifanyiwa vipimo vya damu siku ya Jumatano na matokeo ya vipimo yalikuwa ya kawaida. Kupunguzwa kwa taratibu za oksijeni kunaendelea na anaadhimisha ibada za Misa kila siku katika kikanisa.Hakuna ziara kwa sasa,mapumziko,matibabu na shughuli kidogo za kazi zinaendelea.Ndiyo taarifa iliyosasishwa Ijumaa 28 Machi 2025 kutoka Ofisi ya Vyombo vya habari,Vatican.

Vatican News

Ijumaa tarehe 28 Machi 2025, taarifa kutoka Ofisi ya vyombo vya habari, imesasisha kuhusu afya ya Papa  Francisko kwamba:

"Hali ya afya ya Papa inaendelea kupata nafuu kwa mtazamo wa kupumua na mazoezi ya viungo na hata kwa upande wa kuzungumza. Kuna upunguzaji wa kutumia oksijeni ya mtiririko wa juu wa kutumia mirija ya pua kwa siku na kupunguzwa ile ya usiku. Vipimo vya damu ni vya  kawaida kulingana na matokeo ya vipimo vilivyofanywa Jumatano tarehe 26 Machi. Papa anabadilishana siku  kati ya matibabu ya dawa, sala, kupumzika kidogo na shughuli zake. Mabaraza yote ya kipapa yanamtumia hati. Hakuna ziara zozote maalum zilizopangwa. Amefuatilia mahubiri ya Kwaresima kwa mbali, asubuhi ya Ijumaa tarehe 28 Machi 2025. Tafakari ya Sala ya Malaika wa Bwana itatumwa kama ilivyokuwa Dominika zilizopitia. Papa alitaarifiwa juu ya tetemeko la ardhi nchini Myanmar na yuko anasali kwa ajili ya waathirika wengi. Kila siku anaadhimisha  misa katika kikanisa cha Mtakatifu Marta.”

Sasisho la Afya ya Papa
28 Machi 2025, 14:46