杏MAP导航

Tafuta

Papa Francisko anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Gemelli,Roma. Papa Francisko anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Gemelli,Roma. 

Papa Francisko Hospitalini Gemelli alilala vizuri wakati wa usiku

Taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Vatican kuhusu afya ya Papa.Jana jioni,mawasiliano kwa waandishi wa habari yalifahamisha kwamba hali ya kliniki ya Papa Francisko"alibaki hakuwa na homa na alikuwa macho kila wakati,huku akishirikiana na matibabu na mwelekeo thabiti na kwamba hakukuwa na vipindi vya kushindwa kupumua."

Vatican news

"Papa alilala vizuri wakati wa usiku, akaamka muda mfupi baada ya 2:00." Hii ni taarifa kuhusu hali ya afya ya Papa Francisko, aliyelazwa katika hospitali ya Gemelli, Roma tangu Februari 14, iliyotolewa asubuhi ya leo, tarehe 5 Machi 2025, na Ofisi ya Vyombo vya Habari.

"Asubuhi hii Papa aliendelea na tiba yake na ya viungo vya kupumua. Kama ilivyopangwa, alihamia kutoka uingizaji hewa ya mitambo isiyovamia usiku hadi ya utiririshaji wa oksijeni ya juu kwa kutumia pua. Hali inaonekana kuwa thabiti, kila wakati katika muktadha wa hali tete."

Jana jioni Jumanne tarehe 4 Machi 2025, taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Vatican ilibanisha:  "Leo hali ya kimatibabu ya Baba Mtakatifu iliendelea kuwa shwari. Hakuwasilisha matukio ya kushindwa kupumua au (bronchospasm)kupumua papo hapo. Amebaki bila homa, daima akiwa macho, akishirikiana katika tiba na mwelekeo.

Asubuhi ya leo alibadilishiwa tiba ya oksijeni ya mtiririko wa juu na akafanyiwa mazoezi ya kupumua. Leo usiku, kama ilivyopangwa, atapewa hewa ya mitambo isiyovamia hadi kesho asubuhi. Utabiri unabaki kuhifadhiwa.

Wakati wa mchana alibadilishana na muda wa kusali na  kupumzika na asubuhi ya leo alipokea Ekaristi."

Sasisho saa 9.10 alasili Jumatano 5 Machi 2025.

05 Machi 2025, 08:43