杏MAP导航

Tafuta

Basi lililoanguka chini ya daraja huko Guatemala,Amerika ya Kati. Basi lililoanguka chini ya daraja huko Guatemala,Amerika ya Kati.  (AFP or licensors)

Telegramu ya Papa ya rambirambi kwa waathirika wa ajali ya Bus huko Guatemala

Papa alituma telegram iliyotiwa saini na Kardinali Parolin,Katibu wa Vatican kwa Askofu Mkuu Gonzalo de Villa wa Vasquez,mji wa Santiago ya Guatemala,akitoa salamu zake za rambirambi kufuatia na vifo vya zaidi ya 50 vilivyosababishwa na ajali ya chombo cha usafiri kwenye korongo mnamo tarehe 10 Februari 2025.

Vatican News

Mauaji ya kutisha, zaidi ya mita 100 chini ya bonde na vifo karibia  abiria 55 kati ya 75 katika ajali iliyotokea tarehe 10 Februari 2025, wakati wa kusafiri kwenye daraja nje kidogo ya mji mkuu wa Guatemala,  Bus lililojaa liliruka kando ya barabara ya kitongoji cha Atlántida na likaanguka ndani ya mto wa maji na kuvunjika chini ya maji. Theluthi mbili za watu waliokuwemo ndani ya Bus hilo wakiwemo watoto walifariki  na wengi wakijeruhiwa vibaya.

Mshikamano wa Papa

Ni katika mkutadha huo ambapo Baba Mtakatifu Francisko Ijumaa tarehe 14 Februari ameonesha kuhuzunika sana kufuatia na taarifa hiyo ya ajali na kutaka kueleza mshikamano wake kupitia  telegramu iliyotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin katibu wa Vatican , iliyoelekezwa kwa Askofu Mkuu Gonzalo de Villa y Vasquez, wa Mjini wa  Santiago ya  Guatemala. Katika maandishi hayo Papa, anatoa maombi yake kwa ajili ya mapumziko ya milele ya marehemu na rambirambi zake kwa familia, pamoja na wasiwasi wake mkubwa na matashi  yake ya kupona haraka kwa majeruhi.

Maombelozi ya siku tatu ya kitaifa

Katika maelezo mapya ya tukio hilo kutoka kwa wazima moto, wanabainisha kuwa Bus hilo lililokuwa limejaa ambalo lilianhuka kutokana na kugongana kati ya magari kadhaa muda mfupi kabla ya mapambazuko ya siku ya Jumatatu. Rais Bernardo Arevalo  wa Nchi hiyo alitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Rambi rambi za Papa huko Guatemala
14 Februari 2025, 16:51