杏MAP导航

Tafuta

Maandamano ya Toba,Misa Takatifu ya  Kupakwa Majivu Maandamano ya Toba,Misa Takatifu ya Kupakwa Majivu  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Ratiba za kipapa kwa mwezi Machi na Aprili 2025:Mafungo ya kiroho mjini Vatican

Katika ratiba ya sherehe zikazoongozwa na Papa Fransisko kwa mwezi Machi na Aprili,kama ilivyotangazwa na Askofu mkuu Diego Ravelli,Mhehereshaji wa Liturujia za Kipapa,pamoja na mambo mengine kuanzia tarehe 9 hadi 14 Machi kutafanyika Mafungo ya kiroho kwa maandalizi ya Pasaka kwa Papa na Curia Romana katika Ukumbi wa Paulo VI.Jubilei za Ulimwengu wa Kujitolea na Wagonjwa na Ulimwengu wa Huduma ya Afya zimepangwa katika Mwaka Mtakatifu.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Askofu Mkuu Diego Ravelli, Mshehereshaji wa Liturujia za Kipapa, Jumatano tarehe 12 Februari 2025, amechapisha ratiba ya maadhimisho yanayotarajiwa kuongozwa na Baba Mtakatifu Francisko kwa mwezi Machi na mwanzoni mwa Aprili 2025.

Jumatano ya Majivu, 5 Machi

Katika ratiba hiyo ya maadhimisho ambayo Baba Mtakatifu anatarajia kwa siku zijazo, ni kuanzia na tarehe 5 Machi  2025 ambayo ni Jumatano ya Majivu. Katika Kanisa la Mtakatifu Anselmi saa 10.30  jioni, itafanyika  maandamao ya toba hadi  Basilika ya Mtakatifu Sabina ambapo  saa 11.00 majira ya jioni, Misa Takatifu itafanyika kwa baraka na kupakwa majivu.

Jubilei ya Ulimwengu wa Watu wa kujitolea, 9 Machi

Tarehe 9 Machi, itakuwa ni Dominika ya Kwanza ya Kwaresima ambapo, katika Uwanja wa Mtakatifu Petro saa 4.30  majira ya asubuhi,  itaathimishwa  Misa Takatifu  kwa ajili ya Jubilei ya Ulimwengu wa Watu wa Kujitolea

Mwanzo wa mafungo ya kiroho  ya Papa na Curia Romana, 9-14 Aprili

Na tarehe hiyo hiyo 9  pia itakuwa ni mwanzo wa Mafungo ya kiroho ya Baba Mtakatifu na Wahusika wa Curia Romana itakayofanyika katika Ukumbi wa Paulo VI saa 11.00 jioni. Hadi tarehe 14 Machi 2025  itahitimishwa Mafungo  ya kiroho ya Baba Mtakatifu na Wajumbe wa Curia Romana katika Ukumbi wa Paulo VI mjini vatican saa 3.00 asubuhi.

Jubilei ya wagonjwa na Ulimwengu wa Huduma ya Afya, 6 Aprili

Tarehe 6 Aprili 2025 itakuwa ni Dominika ya V ya Kwaresima ambapo katika Uwanja wa Mtakatifu Petro mjini Vatican saa 4.30 itaadhimishwa misa Takatifu ya “Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa Huduma ya Afya kwa Mwaka Mtakatifu.

Ratiba ya Papa kwa mwezi Machi na Aprili 2025
12 Februari 2025, 15:25