杏MAP导航

Tafuta

Migogoro inaendelea Palestina na Israeli. Migogoro inaendelea Palestina na Israeli.  (AFP or licensors)

Papa Francisko:Tuziombee nchi zilizo katika vita na tukumbuke watu waliokimbia makazi,Palestina

Mwishoni mwa Katekesi yake Papa alisisitiza ombi lake kuhusu maeneo yanayoteseka kwa sababu ya migogoro na wazo maalum kwa watu waliohamishwa kutoka Palestina.Papa pia alihimiza kuwa tuwaombee mapadre na watawa wanaofanya huduma yao huko Ukraine,Mashariki ya Kati na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo:'uwepo wao ni uthibitisho kwamba Mungu anawakumbuka watu wake.'

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Kama kawaida yake, Baba Mtakatifu Francisko katika Katekesi yake tarehe 5 Februari 2025 katika Ukumbi wa Paulo VI hakukosa kukumbuka nchi zilizogubikwa na migogoro na matokeo yake mabaya. Licha ya kuwa na mafua ambayo yalimzuia hasisome katekesi yake kwa kumkabidhi Padre Pierluigi Giroli, Mkuu wa ofisi ya Sekretarieti ya Vatican, Baba Mtakatifu alipenda hata hivyo “kutamka mwenyewe Wito kwa ajili ya Nchi ambazo zinateseka na vita”

“Na tunafikiria nchi zinazoteseka kwa sababu ya vita: Ukraine inayoteswa, Israeli, Jordan ... Kuna nchi nyingi zinazoteseka huko. Tunawakumbuka watu waliokimbia makazi yao huko Palestina na tunawaombea," Papa alisema.

Maombi kwa Mapadre katika Nchi Maskini au Vita-Katika Vita

Hata katika salamu zake kwa mahujaji wa Poland, Papa alitaja maeneo yaliyokumbwa na umaskini au vurugu, akiwahimiza "kuombea mapadre na watu waliowekwa wakfu ambao wanatekeleza huduma yao katika nchi maskini na zilizoharibiwa na vita," hasa "huko Ukraine, katika Mashariki ya Kati na katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo".

Salamu kwa mahujaji

Ninawakaribisha kwa moyo mkunjufu mahujaji wanaozungumza Kiitaliano. Kwa namna ya pekee, nawasalimia wanahija ya Jimbo la Mazara dya Vallo pamoja na Askofu Angelo Giurdanella; Ninawasalimu waamini wa Mtakatifu Angelo huko Esca, kituo cha Benedikto  XVI cha  Buccinasco na wanafunzi wa shule ya Mtakatifu  Paolo ya Pogliano Milano. “Ninatumaini kwamba kutembelea makaburi ya Mitume kutachochea katika jumuiya zenu hamu mpya ya kuambatana na Kristo na kutoa ushuhuda wa Kikristo.”

“Hatimaye, mawazo yangu yanawaendea vijana, wagonjwa, wazee na wenye ndoa za hivi  karibuni. Kama vile mtume Paulo anavyohimiza, ninawatia moyo muwe na furaha katika tumaini, hodari katika dhiki, mkidumu katika kuomba, mkizingatia mahitaji ya ndugu zenu ( Warumi 12:12-13). Baraka yangu kwa wote,” Papa alisema.

05 Februari 2025, 16:12