杏MAP导航

Tafuta

Papa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Gemelli Papa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Gemelli  (ANSA)

Papa amelala salama usiku na yupo anapumzika

Taarifa ya asubuhi ya leo,Februari 26,kuhusu afya ya Papa aliyelazwa katika hospitali ya Gemelli:“Papa amelala salama usiku na yupo anapumzika” ilitolewa na Ofisi ya Vyombo vya Habari,Vatican na ambapo jana jioni,Februari 25 ilitoa maelezo kuhusu hali ya kliniki ya Papa Francisko,ambayo"imesalia kuwa tete,lakini thabiti"na hakuna matukio ya kupumua kwa haraka na vigezo vya vipimo vya damu vinaendelea kuwa thabiti na ubashiri unabaki kuhifadhiwa.”

Vatican News

“Papa alilala usiku kucha kwa utulivu na yupo anapumzika.” Ndivyo maelezo ya asubuhi hii Jumatano saa 2.06 saa za Ulaya na saa 4.06 Masaa ya Afrika Mashariki na kati tarehe 26 Februari 2025 yaliyotolewa katika Ukumbi wa Vyombo vya habari vya Vatican katika taarifa kwa waandishi wa habari.

Hata hivyo Jumanne jioni tarehe 25, Februari 2025 taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya habari vya Vatican ilisasisha kuhusu afya ya Baba Mtakatifu Francisko aliyelezwa tangu tarehe 14 Februari 2025  katika Hospitali ya Gemelli, Roma ikibainisha kuwa "hajapata matatizo ya kupumua, na vigezo vyake vya damu bado ni thabiti. Utabiri unabaki kulindwa.

Jioni hii Papa alifanyiwa uchunguzi wa X-ray uliopangwa kwa ajili ya ufuatiliaji wa picha ya ugonjwa wa mkamba wa sehemu mbili na Utabiri unabaki kuhifadhiwa. Asubuhi ya Jumanne Februari 25, mara baada ya kupokea Ekaristi, aliendelea na shughuli zake za kazi."

 

 

26 Februari 2025, 08:43