杏MAP导航

Tafuta

Kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2025:kitaanza na Jumatano ya majivu tarehe 5 Machi. Kipindi cha Kwaresima kwa mwaka 2025:kitaanza na Jumatano ya majivu tarehe 5 Machi. 

Kwaresima,Kard.De Donatis ataongoza Liturujia ya Majivu huko Aventino,Roma

Ofisi ya Maaadhimisho ya Liliturujia za Kipapa imetangaza kwamba,kutokana na kulazwa kwa Papa katika hospitali ya Gemelli,Mhudumu Mkuu wa Toba ya Kitume,Kardinali De Donatis ataongoza maadhimisho ya Jumatano ya majivu kuashiria mwanzo wa maandalizi ya Pasaka.Liturujia itafanyika katika Kanisa la Mtakatifu Anselmi huko Avventin,kwa kufuatia maandamano ya toba kuelekea Basilika ya Mtakatifu Sabina ili kuadhimisha misa Takatifu.

Vatican News


Siku ya Jumatano tarehe 5 Machi 2025, itakuwa ni siku ya kuanza kipindi cha Kanisa cha Kwaresima kwa mwaka 2025, kwa kupakwa majivu, kuashiria mwanzo wa wakati wa maandalizi ya Pasaka, ambapo saa 10.30 jioni masaa ya Ulaya na saa 12.30 jioni masaa ya Afrika Mashariki na Kati, Kardinali Angelo De Donatis, Mhudumu mkuu wa Toba ya Kitume na Mwakilishi wa Papa Francisko, kutokana na kulazwa kwake katika Hospitali ya Gemelli, ataongoza liturujia hiyo katika Kanisa la Mtakatifu Anselmi huko Aventino, ambayo itafuatiwa na maandamano ya toba kuelekea katika Basilika ya Mtakatifu Sabina, Roma


Hiyo ni taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Maadhimisho ya Liturujia za Kipapa, Ijumaa tarehe 28 Februari 2025. Maandamano hayo yatahudhuriwa na makadinali, maaskofu wakuu, maaskofu, watawa Wabenediktini wa Mtakatifu Anselmi, Mapadre wadominikani wa Mtakatifu Sabina na baadhi ya waamini. Mwishoni mwa maandamano, hayo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Sabina, sherehe ya Ekaristi itafanyika kwa ibada ya kubariki na kupakwa majivu.

 

28 Februari 2025, 16:33