杏MAP导航

Tafuta

Papa anarudia kukutana wakleri  wa Roma tarehe 6 Machi 2025 Papa anarudia kukutana wakleri wa Roma tarehe 6 Machi 2025  (Vatican Media)

Papa Francisko atakutana na mapadre wa Roma tarehe 6 Machi

Baba Mtakatifu anarudia kukutana na mapadre wake katika Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano.Na utamaduni wa Alhamisi ya kwanza ya kipindi cha Kwaresima utapaishwa.

Vatican News

Baada ya kukutana na mapadre wa Jimbo kuu la Roma mwishoni mwa 2023 na miezi ya kwanza ya 2024, kutokana na baadhi ya mikutano iliyoandaliwa katika majimbo ya sekta mbalimbali za jiji la Roma, Baba Mtakatifu Francisko anarejea tena kukutana na mapadre wake wote Alhamisi tarehe 6 Machi 2025 katika Basilika ya Mtakatifu Yohane huko  Laterano.

Jimbo la Roma lilitangaza hayo huku likisisitiza kwamba mapokeo ya kiutamaduni ya Alhamisi ya kwanza ya kipindi cha Kwaresima yanafanywa kwa upya.

Mkutano wa mwisho na mapadre wa jimbo, watawa na mashemasi wa kudumu katika huduma ya kichungaji ya  jimbo la Roma ulifanyika kunako tarehe 13 Januari 2024.

Machi 6 Papa atakutana na mapadre wa Roma
31 Januari 2025, 18:08