杏MAP导航

Tafuta

Ndege ya Shirika la Ndege la Marekani na Helikopta ya Black Hawk  zilianguka karibu na Uwanja wa Ndege wa Kitaifa wa Reagan. Ndege ya Shirika la Ndege la Marekani na Helikopta ya Black Hawk zilianguka karibu na Uwanja wa Ndege wa Kitaifa wa Reagan.  (2025 Getty Images)

Papa Francisko aonesha huzuni kufuatia Ajali ya Ndege huko Washington

Papa amwandikia Rais Trump wa Marekani kueleza ukaribu wa kiroho kwa wale waliohusika katika mgongano kati ya ndege ya kibiashara na helikopta ya kijeshi karibu na Uwanja wa Ndege wa Ronald Reagan,ambao ulisababisha vifo vya makumi ya watu.

Vatican News

Baba Mtakatifu Francisko, tarehe 30 Januari 2025, katika telegramu aliyoituma kwa Rais wa Marekani, Donald Trump alionesha "ukaribu wake wa kiroho" kwa wale walioathiriwa na ajali iliyotokea huko Washington, kwenye Mto Potomac, karibu na Uwanja wa Ndege wa Ronald Reagan kati ya helikopta ya kijeshi, ikiwa na askari watatu, na ndege ya kibiashara iliyokuwa na abiria 60 na wafanyakazi 4, ambazo ziligongana kwa sababu ambazo bado hazijawekwa wazi na zote mbili zilianguka.

Waokoaji waliojishughulisha na uokoaji wa miili hiyo hawakuelezea kama wangepata manusura na waliripoti kuwa hali ya kazi ni ngumu sana na huenda itachukua siku kadhaa. “Nikizikabidhi roho za marehemu kwa rehema na upendo za Mwenyezi Mungu, ninatoa rambirambi zangu nyingi kwa familia ambazo sasa zinaomboleza kifo cha mpendwa wao,” aliandika Papa Francisko, ambaye alihakikishia sala zake “pia kwa wale waliohusika katika jitihada,”huku aliliombea taifa zima baraka za Mwenyezi Mungu  na  faraja na nguvu.”

Papa Rambi rambi
30 Januari 2025, 17:41