杏MAP导航

Tafuta

2023.10.07 Misa takatifu kwa ajili ya kikosi cha ulinzi cha Vatican. 2023.10.07 Misa takatifu kwa ajili ya kikosi cha ulinzi cha Vatican.  (Vatican Media)

Papa Francisko: Mkristo anapigana na shetani ambaye anataka kuharibu kila kitu

Katika kumbukizi la Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu,Papa aliongoza Misa kwa ajili ya kikosi cha Ulinzi wa Vatican kwenye Groto ya Bikira Maria wa Lourdes.Akitoa tafakari kuhusu liturujia ya Dominika,Papa alizungumza kuhusu maisha sawa na shamba la mizabibu.Ni lazima tuwe makini na kutunza maisha ya kila mmoja wetu ili matawi mabaya yasiingie.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Jumamosi jioni tarehe 7 Oktoba 2023 ikiwa Mama Kanisa anakumbuka Bikira Maria wa Rozari, Baba Mtakatifu  Francisko aliongoza Ibada ya Misa Takatifu mjini  Vatican kwa ajili ya Kikosi cha Ulinzi wa Mji wa Vatican, katika Uwanja wa Groto ya Lourdes iliyoko kwenye bustani ya Vatican. Kikundi hili cha Ulinzi wa mji wa Vatican  kilikuwa kinamkumbuka Somo wao, Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu iliyoaadhimishwa  tarehe 29 Septemba iliyopita.  

Misa katika Groto ya Bikira Maria mjini Vatican
Misa katika Groto ya Bikira Maria mjini Vatican   (Vatican Media)

Katika mahubiri, Papa Fransisko alilinganisha kazi ya askari na shamba la mizabibu ambalo adui, kama ilivyoelezwa katika somo la kwanza kutoka katika Kitabu cha Isaya (Isa 5:1-7), kulingana na liturujia ya Dominika ya XXVII ya kawaida, wakati, giza linaingia ili kuharibu kile kilichopandwa huko. Shamba la mizabibu pia ni picha ya maisha ya kila mtu ambapo wema na uovu hupambana kati yao, Papa Francisko alisema. Bwana ametupanda sisi sote, kana kwamba tulikuwa matawi ya shamba zuri la mizabibu, lakini adui huja kutuharibu daima. Haya ni mapambano ya kila siku: yako na yangu na sisi sote. Mtu ambaye hajisumbui si Mkristo, asiyepata majaribu si Mkristo.

Misa mbele ya Groto ya  Lourdes katika Bustani za Vatican
Misa mbele ya Groto ya Lourdes katika Bustani za Vatican   (Vatican Media)

Kwa hiyo Papa alisema lazima tulinde shamba la mizabibu la kila mmoja wetu. Sisi sote, Papa aliendelea, ni wadhambi, lakini tunataka kusonga mbele na kwa hiyo tunapaswa kupambana na shetani ambaye anataka kuingia katika maisha yetu. Papa akikimbusha kwamba Malaika Mkuu Mikaeli husaidia katika vita hivyo alihimiza kuwa: Lazima tuwe makini na kulinda shamba la mizabibu: shamba la mizabibu la kila mmoja wenu, shamba la mizabibu la familia zenu, la watoto wenu na shamba la mizabibu, hapa, mko Vatican, ili pasiwepo  matawi mabaya ya kuingia.

Wakati wa matoleo ya vipaji
Wakati wa matoleo ya vipaji   (Vatican Media)

Katika Kifungu cha Injili ya Mathayo (Mt 21:33-43) ambacho kinatoa mfano wa wakulima walioamua kumiliki kile ambacho walikabidhiwa, Papa alisema kinatuambia kwamba shetani anapotaka kumiliki kitu anakiharibu. Vita ambayo inataka kuharibu kila kitu ni vita chafu, na kwamba  shetani anajaribu kushinda kwa kuharibu. Lakini Mtakatifu Mikaeli  hutusaidia kumfukuza.

Papa misa katika Groto ya Lourdes
08 Oktoba 2023, 10:20