杏MAP导航

Tafuta

Papa amkeutana na kikundi cha watu wa imani tofauti na madhehebu ya Kikristo wanaoshiriki katika shughuli za Kanisa la Ureno. Papa amkeutana na kikundi cha watu wa imani tofauti na madhehebu ya Kikristo wanaoshiriki katika shughuli za Kanisa la Ureno.  (ANSA)

Papa:njia ya mazungumzo na udugu kati ya dini ni muhimu!

Kipindi muhimu cha mazungumzo ya kina ya kiekumeni na ya kidini umemwona Papa Francisko huko Lisbon mara baada ya kuhitimisha ratiba ya asubuhi ya siku ya III ya uwepo wake nchini Ureno.Ni kukutana na wajumbe wa Kituo cha mashirika baina ya serikali KAICIID na kikundi cha watu wa imani tofauti na madhehebu ya Kikristo,Ureno.

Vatican News

Mwishoni mwa asubuhi ya mikutano ya kwanza, tarehe 4 Agosti 2023, Baba Mtakatifu Francisko aliporudi Ubalozini, baada ya mkutano na wawakilishi wa baadhi ya vituo vya misaada na Caritas katika Kituo cha Parokia ya Serafina, alipata ugeni wa ujumbe kutoka kituo cha kimataifa cha mazungumzo KAICIID, wakiambatana na Kardinali Miguel Ángel Ayuso Guixot, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Majadiliano ya Kidini. Katika salamu za wajumbe hao Papa Francisko alitoa shukrani zake kwa ziara hiyo na kusema  maneno machache kwa waliohudhuria juu ya thamani ya udugu na mazungumzo na juu ya hatari ya kujifungia na kugeuza imani.

Baadaye, Papa alifanya mazungumzo na Rahim Aga Khan, mtoto wa  kiongozi wa jumuiya ya Waishmaeli, ambayo ina kituo chake huko Lisbon.

Papa pia alipokea kikundi cha watu wa kidini na wa imani tofauti na madhehebu ya Kikristo wanaohusika katika kujitolea kwa ajili ya  uekumeni na kidini kwa Kanisa la Ureno. Baba Mtakatifu Francisko amewashukuru wale waliohudhuria kwa ajili ya udugu wenye uzoefu, kwa juhudi za mazungumzo, na kutoa pendekezo la  kuwatunza vijana, ambao alisisitiza, ni wachangamfu, lakini sio wa juu juu, na wana hatari ya kugandishwa na ulimwengu unaowazunguka.

Papa amekutana na wajumbe wa shirika baina ya serikali KAICIID walioko Ureno.
Papa amekutana na wajumbe wa shirika baina ya serikali KAICIID walioko Ureno.   (ANSA)

Hatimaye, kabla ya chakula cha mchana, Papa alikutana kwa muda mfupi na mwandishi wa habari wa Israel Henrique Cymerman.

04 Agosti 2023, 18:19