杏MAP导航

Tafuta

Familia ya Carlo Acutis wakisalimiwa na Papa Leo XIV wakati wa Misa kutangazwa kwa Carlo Acutis. Familia ya Carlo Acutis wakisalimiwa na Papa Leo XIV wakati wa Misa kutangazwa kwa Carlo Acutis.  (ANSA)

Ushuhuda wa Mama wa Acutis:Carlo anagusa mioyo ya wengi ni daraja linalopeleka kwa Yesu

Katika siku ya Kutangazwa Mtakatifu wa mtoto wa Antonia Salzano,alisimulia hisia kali iliyobaidlisha maisha yake na familia yake.Wengi wanapata uongofu kwa kutazama mifano yake ya kukumbuka,na nzuri sana ni ile ya ukarimu wa upendo kwa Mungu na kwa wengine!

Na Daniele Piccini – Vatican.

Ni vigumu kufikiria hisia za mama kuona utakatifu wa mwanawe ukitangazwa mbele ya makumi ya maelfu ya watu, akijua kwamba mamilioni ya watu duniani kote wanamwomba na kumshikilia katika mioyo yao. Antonia Salzano, mama yake Carlo Acutis, alikuwepo tarehe 7  Septemba 2025, pamoja na mumewe na watoto wake wengine wawili katika Misa ya kutangazwa kuwa Mtakatifu iliyoongozwa na Papa Leo XIV. Na katika fursa hiyo alishiriki na vyombo vya habari vya Vatican kuhusu safari ambayo imetokea kwa miaka mingi, na kuhitimishwa na sherehe katika uwanja wa Mtakatifu Petro.

La mamma di Carlo Acutis, Antonia Salzano Acutis.

Mama wa Carlo Acutis, Antonia Salzano Acutis.

Bi Acutis, ulipataje uzoefu masaa ya kabla ya Misa ya kutangazwa kuwa Mtakatifu?

Nina furaha kwa sababu hakika ni kilele cha safari ambayo imechukua miaka mingi, ambapo tumepokea maajabu mengi ya ajabu kutoka kwa Carlo. Kila siku, tunapokea habari za miujiza na uwongofu. Kwa hiyo waamini hakika watafurahi sana. Nimefurahiya, lakini pia utulivu na ukimya, kwa sababu kutangazwa kuwa mtakatifu kutakuwa na matokeo  ambayo waamini wote wamekuwa wakingojea. Carlo ana waamini ulimwenguni pote, kutoka Uchina, Japan, Marekani, Amerika Kusini. Nina furaha hasa kwa ajili yao. Ninaamini Carlo anagusa mioyo ya watu wengi, maisha mengi, kwa mfano wake, kwa imani yake ya kuambukiza, na hii inanifurahisha sana.

Je, kuna kumbukumbu fulani ya mwanao inayokuja akilini kwa msisitizo zaidi wakati huu?

Carlo aliacha nyuma kumbukumbu nyingi nzuri, imani yake kuu, kujitolea kwake sana. Nakumbuka kwamba alipokuwa akiandaa maonesho ya Miujiza ya Ekaristi, alikuwa na wasiwasi. "Kuna mistari ambayo ni mirefu ya kilometa kadhaaa  mbele ya tamasha, mbele ya mchezo wa kandanda," alisema, "lakini sioni mistari hii mbele ya hema ambapo maisha na uwepo halisi wa Kristo upo." Na ninakumbuka akifanya kazi, nilipokuwa likizo, hadi saa mbili au tatu asubuhi, na mama yangu, ambaye alilala naye, alimwambia: "Lakini Carlo, acha Kanisa lifanye mambo haya!" Lakini alitumia kila msimu wa kiangazi kuandaa vitu. Alihakikisha watu wanaelewa umuhimu wa Ekaristi. Kumbukumbu yangu ya kupendeza ya Carlo hakika ni ukarimu huu, upendo huu kwa wengine na, zaidi ya yote, kwa Mungu.

L'immagine di Carlo Acutis sulla facciata della Basilica vaticana

Picha ya Carlo Acutis mbele ya Basilika ya Vatican (@Vatican Media)

Unafikiriaje maisha yako kuanzia kesho?

Maisha yangu ya imani daima yatakuwa sawa. Maisha ni safari ya kuelekea utakatifu. Natumaini sisi pia tunaweza kuendelea, kwa sababu sote tumepungukiwa, tuko kwenye safari, marudio yetu ni mbinguni. Lakini maisha yanaleta vikwazo, udhaifu, tuna vingi sana. Ningependa kuwa na neema hizo za kutosha kunisaidia mimi na familia yangu. Ningependa kuweza kufuata njia hii ya utakaso, pia. Lakini ningependa wafuasi wote wa Carlo wapokee neema hii pia. Yeye anasaidia kuwa kama daraja, daraja la kumfikia Yesu.

Ushuhuda wa mama wa Carlo Acutis
08 Septemba 2025, 09:19