杏MAP导航

Tafuta

2023.01.28 Askofu Mkuu Aldo Berardi, Mwakilishi wa Kitume katika Ghuba ya Arabia na Kuwait. 2023.01.28 Askofu Mkuu Aldo Berardi, Mwakilishi wa Kitume katika Ghuba ya Arabia na Kuwait. 

Asia/Bahraini:Askofu Mkuu Berardi:Papa Leo XIV,ishara ya matumaini na umoja

Kwa kuchaguliwa kwa Papa mpya Leo XIV tarehe 8 Mei,Mwakilishi wa Kitume wa Ghuba ya Arabia alisema:"ni ishara ya matumaini ambayo yanaongeza nguvu ya umoja wetu na Kanisa la Ulimwengu.Na tunathibitisha tendo la upole na lenye nguvu la Roho Mtakatifu,ambaye anaendelea kuliongoza Kanisa katika nyakati za kufanywa upya na utume.”

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Mwakilishi wa Kitume wa Ghuba ya Falme za Arabia Kaskazini, Askofu Mkuu Aldo Berardi, O.SS.T., alibainisha kwamba: “Kwa Kanisa katika Ghuba ya Arabia, wakati huu unaleta faraja mpya tunapoendelea kuishi na kutoa ushuhuda wa Injili, mara nyingi kwa njia za kimya au siri. Alisema hayo mara baada ya kusikia habari za kuchaguliwa kwa Papa Leo XIV kwenye kiti cha upapa tarehe 8 Mei 2025. Mwakilishi wa kitume huyo alisisitiza kuwa: “Katikati ya uhalisia wetu wa kipekee, kuchaguliwa kwa Baba Mtakatifu ni ishara ya matumaini na ushirika, ambayo inaimarisha umoja wetu na Kanisa la kiulimwengu. Wito wake wa amani, mazungumzo na kukutana unasikika kwa undani mioyoni mwetu, hasa katika eneo hili, ambalo maadili haya hayatakiwi tu, lakini ni muhimu.

Mwakilishi wa kitume wa Ghuba ya Arabia Fr Aldo Berardi
Mwakilishi wa kitume wa Ghuba ya Arabia Fr Aldo Berardi

Tunaungana na Baba Mtakatifu katika utume wake wa kujenga madaraja, kukuza upatanisho, kuitisha mazungumzo na kutangaza Injili hadi miisho ya dunia. Tunathibitisha kujitolea kwetu kuwa ishara hai ya ushirika, kuchangia utume wa Kanisa kwa ulimwengu wote kutoka kwa Vicariate yetu katikati ya Ghuba  ya Arabia. “Kwa kuchaguliwa kwa Papa Leo XIV, tunathibitisha tendo la upole na lenye nguvu la Roho Mtakatifu, ambaye anaendelea kuliongoza Kanisa katika nyakati za kufanywa upya na utume. Wakati huu kwa hakika ni neema kuu kwa Watu wa Mungu, kutukumbusha kwamba Kristo hudumu daima mwaminifu kwa ahadi yake, kwa sababu alisema: “Mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”(Mt 28:20). Mama Yetu wa Uarabuni, Nyota ya Uinjilishaji Mpya, amwombee, kwa ajili ya Kanisa na kwa watu wote wa Mungu,” alimalizia Mwakilishi wa Kitume.

Papa akipita katikati ya umati wa washiriki wa Jubilei kutoka makanisa ya mashariki
Papa akipita katikati ya umati wa washiriki wa Jubilei kutoka makanisa ya mashariki   (@VATICAN MEDIA)

Ikumbukwe kuwa Askofu Mkuu Aldo Berardi, wa Shirika la Utatu Mtakatifu sana,( O.SS.T) aliteuliwa na Baba Mtakatifu Francisko tarehe 28 Januari 2023 kuwa Mwakilishi wa Kitume wa Arabia ya Kaskasini na Kuwait  na kusimikwa kuwa Askofu tarehe 18 Machi 2023.

Papa akivalishwa skafu ya kihindi
Papa akivalishwa skafu ya kihindi   (@Vatican Media)
Pongezi Papa Leo XIV kutoka Arabia

 

 

15 Mei 2025, 10:27