杏MAP导航

Tafuta

Mkutano wa Baraza la Maaskofu wa Mabaraza ya Maaskofu Barani Ulaya. Mkutano wa Baraza la Maaskofu wa Mabaraza ya Maaskofu Barani Ulaya.   (? CCEE)

Maaskofu wa Ulaya katika sala kwa ajili ya amani ya Ukraine na Nchi Takatifu

Kwa kipindi chote cha Kwaresima,wajumbe wa CCEE wanaungana katika “mnyororo wa Ekaristi” kwa ajili ya kuomba amani ya haki na ya kudumu na kupyaisha wito wa kusali kwa ajili ya afya ya Papa Francisko.

Vatican News

Kuanzia Jumatano ya Majivu tarehe 5 Machi 2025 na kwa kipindi chote cha Kwaresima, Kanisa Barani Ulaya linabaki kukusanyika katika 'Meza ya Ekaristi' ili kuomba amani. Mkutaniko  huo unaohusisha wajumbe wote wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu wa Ulaya(CCEE,) ni kwa kuhusisha kuandaa na kuadhimisha angalau Misa moja ya kuwaombea wahanga wa vita na kuomba kutoka kwa Bwana "amani ya haki na ya kudumu, hasa kwa ajili ya  Ukraine na Nchi Takatifu."

Ishara ya matumaini kwa Ulaya

Tukio hili limepewa mada: “Mnyororo wa Ekaristi” ambalo linalenga kuwa uzoefu wa umoja na ishara inayoonekana ya matumaini kwa Bara zima la Ulaya; kwa wakati wa maombi, kufunga na kutoa sadaka  kwa kujisikia kama sisi sote ni ndugu na kumwomba Mungu kukomesha vita."

Kuomba kwa ajili ya Papa

Katika siku hizi za mateso na magonjwa, aidha walitoa wito mpya kwa waamini wote kuombea afya ya Papa Francisko.

06 Machi 2025, 10:11