杏MAP导航

Tafuta

2025.02.03 TALITHA KUM 2025 2025.02.03 TALITHA KUM 2025 

Siku ya kupinga Biashara haramu ya binadamu:vijana jijini Roma na Talitha Kum!

Katika matazamio ya toleo la XI la Siku ya Sala na Tafakari Ulimwenguni dhidi ya biashara haramu ya binadamu itakayofanyika tarehe 8 Februari,sanjari na Siku kuu ya Mtakatifu Josephine Bhakita,kikundi cha mabalozi vijana kutoka ulimwenguni kote wamekuwa wahamasishaji wa matumaini na silaha ya kutembe kwa hadhi ili kusema hapana matukio haya.

Na Sr Bernadette Reis – Vatican.

Wanatoka Australia, Cameroon, Japan, Albania, Romania, Ukraine, Kenya, Mexico, Uruguay, Peru. Wameungana na  Harakati ya Talitha Kum, mtandao wa kimataifa wa watawa  wanaopambana na biashara haramu ya binadamu, kama mabalozi wa vijana. Juma lao la shughuli ya kuhamasisha jijiji  Roma liilianza Jumamosi tarehe 1 Februari , wakati Dominika saa 6 Mchana waliungana na Papa Francisko katika uwanja wa Mtakatifu Petro kwa ajili ya kusali sala ya Malaika wa Bwana. Kisha, Jumatatu  tarehe 3 Februari mabalozi hawa wa vijana wakawa mahujaji wa matumaini, wakielekea kwenye Basilika ya Mtakatifu Petro, wakitembea kimwili lakini pia kidijitali "wakiwa na silaha" na kutumia Programu ya simu ya kutembea kwa hadhi , kwa lengo la kuwashirikisha hata wengine kila kona ya dunia ambayo ilihesabu kila hatua yao. Hatua ambazo zimevuka kizingiti cha Mlango Mtakatifu na zinazochangia katika mapambano dhidi ya biashara haramu ya binadamu na zitafaidika na mipango mingi ya Harakati ya Talitha Kum iliyoenea duniani kote.

Talitha KUM
Talitha KUM

Siku ya Februari 8

Baada ya lile la Basilika ya  Mtakatifu Petro, vijana hao pia walipitia Milango Mitakatifu ya Mtakatifu Yohane huko  Laterano  na Mtakatifu Maria Mkuu. Siku ya Alhamisi tarehe 6 Februari, watapitia Mlango Mtakatifu wa Basilika ya Mtakatifu Paulo Nje ya Kuta. Sr  Abby Avelino, mratibu wa kimataifa wa Harakati ya Talitha Kum, alisema mabalozi hao vijana wamechukua fursa ya Mwaka wa Jubilei na hija ya matumaini kuwaalika watu wengi kutembea nao, kwa heshima. Wito huu ulizinduliwa hasa wakati wa Juma la shughuli zinazotangulia Siku ya kumi na moja ya Maombi na Tafakari dhidi ya Biashara Haramu ya Binadamu, ambayo itaadhimishwa Jumamosi tarehe 8 Februari 2025,  sambamba na siku kuu ya Mtakatifu Bakhita mwathirika wa Biashara haramu ya Binadamu.

TALITHA KUM
TALITHA KUM   (© Marco Mastrandrea/ Talitha Kum)

Milioni 50 watumwa wa kisasa

Kwa kutumia Programu ya Kutembea kwa Hadhi, mabalozi wachanga wanaweza kutangaza programu kupitia  simu, kuongeza ufahamu kuhusu biashara haramu ya binadamu, na wakati huohuo kuchangia mipango iambayo watawa wameifanya, alieleza Sr Abby.  "Watawa wetu wanafanya kazi katika ngazi ya chini na wanachama 6,000 wa Talitha Kum. Tunapotembea kwa heshima na watu, bado tunafahamu ni watu wangapi bado wanaishi katika hali ya utumwa mamboleo yaani milioni 50 ndio makadirio.” Kutembea pamoja, kwa hivyo, tunaweza kuota na kutumaini kukomesha biashara haramu ya binadamu." Programu ya Kutembea kwa hadhi  ilizinduliwa tarehe 30 Januari 2024  na mabalozi wa vijana wa Talitha Kum. Kupitia hilo, wanawaalika wenzao kushiriki katika kuwahudumia waathiriwa wa biashara hiyo kwa kutembea pamoja. Hatua zao zinapohesabiwa na kuchangiwa, wanaweza kufungua maudhui na kujifunza jinsi Talitha Kum hutekeleza dhamira yake.

VIJANA NA TALITHA KUM
05 Februari 2025, 17:20