杏MAP导航

Tafuta

Maandalizi yanafanyika ili kumpokea Papa Francisko mnamo Septemba ijayo. Maandalizi yanafanyika ili kumpokea Papa Francisko mnamo Septemba ijayo. 

Watoto wa Papua New Guinea watatumbuiza tamasha la dakika 5 kwa ajili ya Papa

Papa Francisk akapotembelea Papua New Guinea mwezi Septemba,kikundi cha watoto 70 kutoka Mpango wa Malkia wa Mbingu watafanya tamasha la dakika 5 kumkaribisha huko Vanimo.Mratibu wa Kikundi alisema“watoto wanafurahi kumtumbuiza Papa na ya sehemu mbili ni “dhahabu safi.”

Vatican News

Baadhi ya watoto 70 kutoka Mpango wa Malkia wa Mbingu (QOP) wameratibiwa kumwimbia Baba Mtakatifu  Francisko katika ziara yake  ya kitume ijayo nchini Papua New Guinea mwezi Septemba 2024. Padre Miguel de la Calle wa kikundi cha Orchestra cha QOP alisema kuwa watoto watacheza ala za muziki na kumwimbia papa mnamo  tarehe 8 Septemba 2024 huko Vanimo. “Watoto wa Bendi ya Mpamgo wa Malkiwa wa Mbingu (QOP) wamefurahi sana, kwani Papa Francisko atawasikiliza ana kwa ana,” Alisema Padre huyo katika ripoti yake kwenye (The National), gazeti la ndani ya nchi hiyo. Padre Miguel alisema watoto hao watamsubiri Papa Francisko mwishoni mwa safari yake ya kilomita 13 ya gofu huko Vanimo ili kuwabariki watu.

Papa licha ya kutembelea kiti cha magurudumu,atakwenda kutembelea watu

Mwalimu Jesus Briceño, ambaye ataongoza kikundi hicho, alielezea tamasha la dakika 5 kama  ni kama “dhahabu safi,” akiongeza kwamba wanatayarisha “vipande viwili vya muziki” kwa ajili ya Papa. Kardinali John Ribat, Askofu Mkuu wa Port Moresby, alielezea ziara ya Papa Francisko huko Papua New Guinea kuwa “baraka.” Askofu Mkuu alibainisha kuwa "Papa anayekuja, sio tu kama kiongozi wa Kanisa Katoliki tu lakini pia kama mkuu wa serikali. “Ningependa kusisitiza kwamba Papa anakuja kama mtu asiye na afya nzuri, na hivyo atakuwa kwenye kiti cha magurudumu. Yeye atafikisha miaka 88 mwaka huu. Katika umri wake na masuala yote yanayozunguka afya yake, bado aliamua kuja.”Alisisitiza kiongozi hiyo. Aidha Kardinali Ribat aliwakumbusha waamini kwamba: "Papa ni mtu kama ninyi na mimi." Hata hivyo, alikazia “ikiwa Yesu Kristo alimchagua afanye kazi hiyo muhimu ulimwenguni, tunahitaji kujitayarisha vyema kwa ajili ya kuja kwake na kumkaribisha.”

Matayarisho ya Watoto nchini Indonesia watakaomwimbia Papa
22 Agosti 2024, 15:09